umojannguvu.blogspot.com

Tuesday 8 September 2015

Kuanza kwa ujenzi wa reli habari njema




WAZIRI wa Uchukuzi, Samuel Sitta alikaririwa juzi na vyombo vya habari, likiwemo gazeti hili, kwamba ujenzi wa Reli ya Kati ambayo imekuwa ikisuasua kwa muda mrefu, utaanza mwezi huu.

Alisema Rais Jakaya Kikwete anatarajia kuweka jiwe la msingi Septemba 15 mwaka huu katika eneo la Soga Mpiji wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani, kuanzisha ujenzi huo rasmi utakaofanywa na Kampuni ya China Railway Construction.
Akasema ujenzi huo utakaotumia miaka minne, utagharimu Sh trilioni 16. Waziri Sitta alikumbusha kwamba mipango ya ujenzi wa reli hiyo, haijaanza sasa, bali ni tangu wizara hiyo ilipokuwa chini ya Dk Harrison Mwakyembe, na kwamba mpango ni kujenga reli ya kisasa itakayowezesha treni kusafiri kwa kilometa 120 kwa saa na kubeba tani milioni 25 kwa mwaka.

Kadhalika, Sitta alisema mbali ya mradi wa Reli ya Kati kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma, ujenzi wa Reli nyingine ya Kusini kutoka Mtwara kwenda Mbamba Bay, pia unatarajiwa kufanyika.

Ingawa Waziri Sitta aliyasema hayo akijaribu kuwaweka sawa Watanzania, baada ya mgombea wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vingine vinne kupitia Ukawa, Edward Lowassa, kudai atajenga reli hiyo, akiwa amesahau kwamba tayari iko kwenye mipango ya kujengwa, kwetu imekuwa ni habari njema.
Ni habari njema kutokana na umuhimu wa reli hiyo ya kati kuwa na manufaa makubwa kwa nchi yetu na imekuja wakati mwafaka, baada ya Serikali ya Awamu ya Nne, kujitahidi katika ujenzi wa barabara nchini.

Mbali na reli hiyo kuwa chachu ya nchi zinazotuzunguka, ambazo hazina bahari kuongeza kupitisha mizigo katika nchi yetu na hivyo kukuza zaidi uchumi wetu, reli hiyo pia itarahisisha usafirishaji wa abiria na bidhaa za hapa nchini.
Kwa sasa bidhaa nyingi kutoka Dar es Salaam kwenda mikoa ya pembezoni kama Mara, Kigoma, Kagera na hata Tabora, zinasafirishwa kwa njia ghali ya barabara na hivyo zinapofika huko zinakuwa ghali pia.

Zipo taarifa kwamba saruji ya kutoka Wazo Hill, Dar es Salaam au kutoka Mbeya inapofika mkoa kama Mara, inakuwa juu kulinganisha na saruji inayotokea nchi jirani za Kenya au Uganda na hii ni kutokana na usafiri ghali wa barabara.

Lakini, pia kwenye vituo ambako reli inakopita, kama inafanya kazi kama ilivyokuwa miaka ya sabini na themanini, inasababisha wananchi kufanya biashara kwa kutoa huduma kwa abiria au wahudumu wa treni na hivyo kukuza uchumi wao pia.
Wakati tukifurahia habari hii njema, tunawakumbusha pia wagombea, wasitoe ahadi ambazo hazitekelezeki au zile ambazo tayari zimo kwenye mipango ya serikali eti kwa lengo tu la kutafuta kura. Ni vyema wagombea wakatafiti hoja zao, kabla ya kuzisema na kuhakikisha hoja wanazosema ni za kweli.

Ni matarajio yetu kwamba kauli ya Waziri Sitta, itasimama kama alivyosema na ujenzi utaanza na kumalizika katika kipindi hicho cha miaka minne. Kadhalika, tunaamini suala la ujenzi wa Reli ya Kati na mengine yaliyo katika utaratibu wa kufanyiwa kazi na serikali, hayatakuwa tena ‘mitaji’ ya kuombea kura.

0 comments:

Post a Comment

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

CHAT BOX

Post zilizo tumwa

Recent Posts Widget

Tangaza Biashara yako mtandaoni

TANGAZA BIASHARA NAMI HAPA KWA BEI NAFUU KABISA

Unaweza kutangaza biashara yako sasa na hlmservice pia uta pata kujua mambo mengi ambayo mbali na biashara yako unaweza ukatengeneza pesa kwa namna moja ama nyingine kama jinsi nilivo elezea katika Makala za nyuma hapo

Wafanya biashara wengi wanatumia mda mwingi namna gani ya kukuza biashara zao ,Ili uweze kufanikiwa kwa kiasi kikubwa unahitaji kuitangaza biashara yako ili kuwa na mtandao mkubwa na wateja wako ,ni vyema ukatangaza biashara yako katika mitandao ili bidhaa zako zijulikane kwa haraka na upesi .

Pia wewe mfanya biashara ukiitaji kuwa na blog yako wasiliana nami kwa mawasiliano hapo chini , bei ni nafuu kabisa

Pia ukiitaji kuitangaza biashara yako kupitia blog yangu bei ni ndogo kabisa huu ni wakati wako wewe mfanya biashara

+255758061575 & +255684860817

henrylameck@gmail.com

henrylameck90@yahoo.com

Tukuyu Tour & Safari

Vadacom Ni Zaidi

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Kilimo Kwanza

Hlm servise

Latest movie

Movies

Computer books

Computer books