umojannguvu.blogspot.com

Tuesday 1 September 2015

Magufuli awaonya maafisa wanaoendeleza ufisadi


Wakati akampeni za kuelekea uchaguzi mkuu ambao unatarajiwa kufanyika octoba 25 mwaka huu  Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi John Pombe Magufuli ametoa onyo kali kwa maafisa walio katika taasisi za serikali  na halmashauri mbalimbali nchini wanaoendeleza na kufumbia,macho maswala ya,Rushwa na vitendo vya ufisadi na kuwa kikwa kwa maendeleo.
Magufuli ambaye ni mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM ambaye pia ni waziri wa Ujenzi  ametoa kauli hiyo wakati akiwahutubia wananchi na wanachama wa chama hicho katika mkutano mkoani Ruvuma wa kampeni zinazoendelea nchini na kudai kupambana na baadhi ya viongozi wasio waadilifu kwa  kutelekeza majukumu yao kikamilifu kuwa atakabiliana nao atakaposhinda uchaguzi mkuu.
Katika kampeni zake mkoani Ruvuma, Magufuli amewaahidi maendeleo wakaazi wa wilaya ya Songea endapo watampa ridhaa ya kuwa Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Dokta Magufuli ameweka wazi msimamo wake wa kukabiliana na ufisadi na uzembe kazini na kuahidi kula nao sahani moja kwakuwa wamekuwa wazembe kazini huku baadhi ya viongozi kufumbia macho viongozi wabadhilifu.


Matamshi yake ya ujasiri yameonekana kuzua msisimko katika mkutano huo wa siasa ambao umefanyika katika uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma ukiambatana na ahadi tele za maendeleo zikiwemo kuimarisha miundo mbinu, afya na elimu ikiwa ni miongoni mwa ahadi alizozipa kipaumbele wakati  akinadi sera za Chama cha Mapinduzi..
Viongozi wa CCM waliohudhuria kampeni hiyo wamewataka wakazi hao kuhakikisha wanawapigia kura wagombea wa chama hicho katika uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 25 mwezi Oktoba mwaka huu.
Source:Startv.
StarTV

0 comments:

Post a Comment

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

CHAT BOX

Post zilizo tumwa

Recent Posts Widget

Tangaza Biashara yako mtandaoni

TANGAZA BIASHARA NAMI HAPA KWA BEI NAFUU KABISA

Unaweza kutangaza biashara yako sasa na hlmservice pia uta pata kujua mambo mengi ambayo mbali na biashara yako unaweza ukatengeneza pesa kwa namna moja ama nyingine kama jinsi nilivo elezea katika Makala za nyuma hapo

Wafanya biashara wengi wanatumia mda mwingi namna gani ya kukuza biashara zao ,Ili uweze kufanikiwa kwa kiasi kikubwa unahitaji kuitangaza biashara yako ili kuwa na mtandao mkubwa na wateja wako ,ni vyema ukatangaza biashara yako katika mitandao ili bidhaa zako zijulikane kwa haraka na upesi .

Pia wewe mfanya biashara ukiitaji kuwa na blog yako wasiliana nami kwa mawasiliano hapo chini , bei ni nafuu kabisa

Pia ukiitaji kuitangaza biashara yako kupitia blog yangu bei ni ndogo kabisa huu ni wakati wako wewe mfanya biashara

+255758061575 & +255684860817

henrylameck@gmail.com

henrylameck90@yahoo.com

Tukuyu Tour & Safari

Vadacom Ni Zaidi

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Kilimo Kwanza

Hlm servise

Latest movie

Movies

Computer books

Computer books