umojannguvu.blogspot.com

Friday 21 August 2015

Chama cha Maendeleo Chadema (Ukawa) sasa yazuiwa kuutumia Uwanja wa Taifa.



Wenyewe wasema hawajapata taarifa zozote zaidi ya kusikia kupitia vyombo vya habari.

Serikali imezuia matumizi ya uwanja wa Taifa kwa shughuli za mikutano ya kisiasa.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Assah Mwambene, (pichani) alisema jana kuwa hatua hiyo imechukuliwa ili uwanja huo utumike kwa shughuli za michezo pekee.

“Tumeamua kuufahamisha umma juu ya jambo hili kutokana na taarifa zilizoenea kwenye mitandao ya kijamii na kuripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) pamoja na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vitafanya mkutano wa uzinduzi wa kampeni keshokutwa katika uwanja huo,” alisema Mwambene.

Alisema walipata barua ya maombi kutoka Chadema Agosti 12 wakiomba uwanja huo kwa ajili ya uzinduzi wa kampeni zao na kwamba walishawapatia majibu kwamba hakuna chama cha siasa kitakachoruhusiwa kutumia uwanja huo kutokana na mihemuko na hamasa za kisiasa inayoweza kujitokeza miongoni wafausi wa vyama na kusababisha uharibifu.

Alisema walichukua uamuzi huo kwa busara ili kuufanya uwanja wa Taifa ubaki kwa ajili ya shughuli za michezo tu.
Hata hivyo, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Chadema, Tumaini Makene, alisema hawajapata taarifa zozote kutoka serikalini zaidi ya kusikia kupitia vyombo vya habari.

Makene aliongeza kuwa hatua hiyo imechukuliwa kuficha aibu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuhofia wingi wa watu
watakaojitokeza kwenye mkutano wa Ukawa kwa kuwa chama tawala kitazindua kampeni zake katika viwanja vya Jangwani eneo ambalo ni dogo ambalo hawawezi kupata watu wengi.

“Serikali inapaswa kutambua kuwa uchaguzi unaamua hatima ya nchi husika kwa kuzingatia demokrasia, hivyo wanachokifanya ni kuvinyima vyama vya upinzani haki ya msingi kwa ajili ya shughuli mhimu kwa kigezo cha kuvunja amani kitu ambacho si sahihi,” aliongeza.

Kwa mujibu wa Makene, hawatapoteza muda kubishana na Serikali bali watatafuta eneo lingine la kufanyia mkutano huo na watatoa taarifa kwa wananchi na wafuasi wote wa Ukawa nchini.

0 comments:

Post a Comment

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

CHAT BOX

Post zilizo tumwa

Recent Posts Widget

Tangaza Biashara yako mtandaoni

TANGAZA BIASHARA NAMI HAPA KWA BEI NAFUU KABISA

Unaweza kutangaza biashara yako sasa na hlmservice pia uta pata kujua mambo mengi ambayo mbali na biashara yako unaweza ukatengeneza pesa kwa namna moja ama nyingine kama jinsi nilivo elezea katika Makala za nyuma hapo

Wafanya biashara wengi wanatumia mda mwingi namna gani ya kukuza biashara zao ,Ili uweze kufanikiwa kwa kiasi kikubwa unahitaji kuitangaza biashara yako ili kuwa na mtandao mkubwa na wateja wako ,ni vyema ukatangaza biashara yako katika mitandao ili bidhaa zako zijulikane kwa haraka na upesi .

Pia wewe mfanya biashara ukiitaji kuwa na blog yako wasiliana nami kwa mawasiliano hapo chini , bei ni nafuu kabisa

Pia ukiitaji kuitangaza biashara yako kupitia blog yangu bei ni ndogo kabisa huu ni wakati wako wewe mfanya biashara

+255758061575 & +255684860817

henrylameck@gmail.com

henrylameck90@yahoo.com

Tukuyu Tour & Safari

Vadacom Ni Zaidi

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Kilimo Kwanza

Hlm servise

Latest movie

Movies

Computer books

Computer books