umojannguvu.blogspot.com

Friday 21 August 2015

Hawa ndio wagombea wanao tarajiwa kuwa na mchuano mkali kwenye uchaguzi mkuu oktoba 25 mwaka huu




 

WAGOMBEA urais wanaotarajiwa kuwa na mchuano mkali kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu, Dk. John Magufuli (CCM) na Edward Lowassa (Chadema), wanarejesha fomu za kugombea nafasi hiyo leo kwenye Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). 

Tofauti ni ilivyokuwa takriban wiki mbili zilizopita wakati wanasiasa hao walipokwenda kuchukua fomu hizo tayari kwa kutafuta wadhamini sehemu mbalimbali nchini, leo watalazimika kwenda kimyakimya. 

Wakati wa kuchukua fomu ambapo Dk. Magufuli ndiye aliyekuwa wa kwanza, shughuli katikati ya Jiji la Dar es Salaam zilisimama kwa muda kuwapisha wanachama wa CCM waliomsindikiza na kisha kuhitimisha kwa hotuba kwenye Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM Mtaa wa Lumumba. 

Siku mbili baadaye, Lowassa naye alifunga mitaa kadhaa ya jiji kwa maandamano yaliyoanzia Buguruni hadi katikati ya jiji, kisha kuelekea Makao Makuu ya Chadema Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, huku Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akishindwa kuhimili mikiki mikiki hiyo na kwenda ‘kupumzishwa’ Muhimbili. 

Kwa kuheshimu shughuli za wakazi wengine wa Dar es Salaam wasiojihusisha na siasa za moja kwa moja, Jeshi la Polisi lilizuia maandamano ya aina hiyo na kuagiza kuwa wagombea hao sasa watasindikizwa na watu saba tu kwenda NEC kurejesha fomu. 

Kwa hiyo leo, Dk. Magufuli (55) ambaye pia ni Waziri wa Ujenzi na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi ya Richmond, Lowassa (62), pamoja na wagombea wa vyama vingine, watarejesha fomu hizo bila mbwembwe zozote.
“Magufuli atawasilisha fomu zake saa tano asubuhi ya kesho (leo) akifuatana na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan,” inasomeka sehemu ya taarifa iliyotolewa jana na CCM. 

Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa ama na Chadema au Ukawakuhusu muda atakaorejeshafomu Lowassa ingawa naye atafanya hivyo leo kwa kuwa ndio siku ya mwishoiliyopangwa na NEC.
Baada ya Dar Magufuli kuanzia Katavi 

Mara baada ya kurejesha fomu, Magufuli atapata fursa ya kuzungumza na Watanzania wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho uliopangwa kufanyika kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam kesho kutwa.
Ingawa bado ratiba rasmi haijatolewa, Raia Tanzania linafahamu kwamba Jumatatu ijayo, Dk. Magufuli ataanza kampeni za mikoani katika Mkoa wa Katavi kisha Rukwa na baadaye Mbeya. 

Kwa upande wa Ukawa, hadi jana jioni hakukuwa na taarifa zozote kuhusu wapi watafanyia uzinduzi wa kampeni na baada ya hapo watakwenda mkoa gani. 

Juzi, ombi la Ukawa kuzinduliz kampeni Uwanja wa Taifa, lilikataliwa na serikali.
Wakati huo huo, NEC imewataka viongozi wa dini nchini kuacha kuonyesha hisia zao juu ya chama au mgombea wanayemtaka na kuepuka kushawishi waumini wao kuegemea upande wowote ili kufanikisha kufanyika uchaguzi wa huru na haki. 

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva, wakati tume hiyo ilipokutana na viongozi wa dini kupeana taarifa kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao. 

Aliwaomba viongozi hao kutumia mimbari kuwaelimisha na kuwafahamisha wapiga kura waweze kufanya uamuzi baada ya kupata taarifa sahihi na kumchagua kiongozi anayemtaka. 

“Ikumbukwe kwamba sheria ya uchaguzi zinakataza viongozi wa dini kutumika katikia masuala ya kisiasa kama vile kufanya kampeni za uchaguzi katika maeneo yenu ya ibada. Kamwe msiruhusu maeneo yenu yatumiwe na vyama vya siasa kama majukwaa ya kisiasa,” alisema Jaji Lubuva.


0 comments:

Post a Comment

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

CHAT BOX

Post zilizo tumwa

Recent Posts Widget

Tangaza Biashara yako mtandaoni

TANGAZA BIASHARA NAMI HAPA KWA BEI NAFUU KABISA

Unaweza kutangaza biashara yako sasa na hlmservice pia uta pata kujua mambo mengi ambayo mbali na biashara yako unaweza ukatengeneza pesa kwa namna moja ama nyingine kama jinsi nilivo elezea katika Makala za nyuma hapo

Wafanya biashara wengi wanatumia mda mwingi namna gani ya kukuza biashara zao ,Ili uweze kufanikiwa kwa kiasi kikubwa unahitaji kuitangaza biashara yako ili kuwa na mtandao mkubwa na wateja wako ,ni vyema ukatangaza biashara yako katika mitandao ili bidhaa zako zijulikane kwa haraka na upesi .

Pia wewe mfanya biashara ukiitaji kuwa na blog yako wasiliana nami kwa mawasiliano hapo chini , bei ni nafuu kabisa

Pia ukiitaji kuitangaza biashara yako kupitia blog yangu bei ni ndogo kabisa huu ni wakati wako wewe mfanya biashara

+255758061575 & +255684860817

henrylameck@gmail.com

henrylameck90@yahoo.com

Tukuyu Tour & Safari

Vadacom Ni Zaidi

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Kilimo Kwanza

Hlm servise

Latest movie

Movies

Computer books

Computer books