umojannguvu.blogspot.com

Saturday 15 August 2015

TECHNOLOGIA YA COMPUTER





 
COMPUTER SERVICES

Karibu tena mtanzania mwenzangu katika tovuti hii mpya ,Utapata habari nyingi zinazo husiana naTechnologia ya sasa.Mimi kama mtanzania mwenzako nimechukua fursa hii kuamasisha watanzania wa leo kutumia zaidi Technologia ya kileo ili kutimiza ndoto zao ,Je Ni vitu gani kuwa navo ili kutimiza ndoto zetu. Pia Kutakuwa na Makala zinazo elezea matumizi mazuri ya computer ,kuteneza home network, bila ya kutumia vifaa vingi na vya gharama,je ni computer gani inafaa kwa matumizi yako,na ipi haifai kwa matumizi yako.Karibu sana wapenzi wasomaji .

SOMA MAKALA MBALIMBALI ZINAZO HUSIANA NA TECHNOLOGIA YA SASA

Moja ya Makala muhimu na watu wengi wanapenda Zaidi ni hasa kujua maisha ya mafanikio yanapatika vipi , je wewe mtanzania wa leo unaitaji kukua kiuchumi . Basi Usikose mada hizi tutakazo kuwa naza katika blog yetu hii Nzuri

kwa leo Nitapenda kukupa Ufahamu Kidogo Kuhusiana na Computer ,


JE COMPUETER NI NINI?


Wewe mtanzania unahitaji kujua computer ni kitu gani kabla ya kuanza kuifanyia kazi pia unabidi kufahamu umuhimu wa kuwa na computer nyumbani kwako ,Leo nitakuwa sijakutendea haki kama sita kufahamisha maana ya computer pamoja na matumizi ya computer ,Kuna maana nyingi sana ya kifaa computer ,utaweza kuelezea maana za computer kutokana na matumizi ya kila siku lakini kwa maana kuu tuta sema kwamba “Computer ni Kifaa kinacho tumia umeme kinacho weza kufanya mambo makuu matatu ambayo ni kuhifadhi data mbali mbali ambazo unaweka ndani ya computer ,Baada ya kuweka data zako katika computer basi zita kuwa processed ndani ya computer na mwisho wa yote tuta pata output ambazo ni matokoe ya data kuwa processed”



Vile vile Computer tutaweza kusema ni kifaa kinacho weza kukurahisishia wewe mtanzania kuingia internet na kufanya shughuli zako mtandaoni mfano mzuri unapo tuma email, unapo chati katika mitandao ya kijamii kama facebook,twiter,nk tutajifunza mengi kuhusu internet endelea kusoma mada hii ili kujua mengi Zaidi ,

Mambo ya msingi kuhusu intaneti 

Wavuti ni nini, na ni jinsi gani unavyoweza kuifanyia kazi?
Unavyochunguza vidokezo juu ya usalama katika Vizuri Kufahamu, unaweza ukawa na maswali kadhaa kuhusu wavuti ni nini na jinsi ya kutumia aina maarufu ya huduma mtandaoni. Tafadhali angalia majibu haya kutoka Googlers na pata maelezo zaidi kuhusu kuingia mtandaoni, kupata maelezo na kuabiri katika mtandao, na kuunganisha na kushiriki mtandaoni.



Kuingia mtandaoni
Intaneti ni nini?

Intaneti ni mtandao wa kompyuta zilizoenea duniani kote zote zikiwa zimeunganishwa moja kwa nyingine. Unapojiunga kwenye Intaneti unakuwa na ufikiaji wa World Wide Web, ambayo ni sawa na maktaba iliyojaa kurasa za maelezo.

Unaunganishwa vipi kwenye Intaneti? Shughuli ya ISP ni ipi?


Kabla hujaanza kuuchunguza mtandao, utahitaji kuweka mpango na ISP. ISP, au Mtoa Huduma za Intaneti, ni kampuni inayokuruhusu kufikia Intaneti na huduma nyingine za mtandao. Wanatoa njia tofauti za kuunganishwa ikiwa ni pamoja na kupiga simu, kebo, fiber optics au Wi-Fi. Muunganisho hizi tofauti huamua kasi ya ufikiaji wako wa mtandao. 
Baada ya kuona maana ya computer na internet basi tuangalie umuhimu wa kuwa na computer ni upi na tutatumia vipi computer kuinua hali zetu za kiuchumi
Computer ina matumizi mengi sana ukiwa nyumbani,kwako mwanafunzi, pia hata maofisini ,pia unaweza ukajiajili kupitia computer yako hapo ulipo
Kwa mwanafunzi utaweza kusomea computer pamoja na kutafuta mengi kwenye internet, kwa mfanya biashara utatunza kumbukumbu zako za kibiasha pia hata za kiofisi
Unaweza kutengeneza pesa kupitia computer yako ya nyumbani kama utakuwa mbunifu wa kujitangaza kupitia computer yako.Blogger ni njia pekee inayo weza kuitangaza biashara yako kwa kasi na kwa watu wengi duniani ,Blog ni mfano wa website ambayo unaweza kuweka matangazo yako ya kibiashara pamoja na kujitangaza wewe ni nani ?
Ni rahisi sana kutengeneza blog yako na kujitangaza Zaidi, pia nitakuelekeza jinsi ya kuanzisha blog yako ya kibiashara pamoja na kupata muonekano mzuri zidi wa blog yako

Mara nyingi unapo tengeneza blog itakulazimu uwe katika internet lakini kuna njia mbali mbali za kutengeneza blog kuonekana katika muonekano mzuri Zaidi kwa kutumia Microsoft word, Microsoft publisher pamoja na Excell, Sio hivo kuna lugha mbali mbali za kutengeneza kurasa za blog yako
Kuna mfano wa lugha ina itwa HTML, CSS, JavaScript ni lugha nzuri za kutengeza kurasa zako za blog yako yote hayo utayapata hapa katika tovuti yetu hii ya hlmservice.

COMPUTER GANI INA FAA KWA MATUMIZI YAKO


Chagua computer inayo weza kukidhi mahitaji yako ukizingatia uwezo wa computer je unahitaji utumie katika matumizi gani, Kwa mfano wewe ni designer na katika designing yako unatumia program kubwa kama adobe photoshop basi chagua computer yenye ukubwa mkubwa kwa kuangalia Hard Disk Isiyo pungua 500Gb na processor 2.20GHz na RAM(Random Access Memory) Sio chini ya 2.0Gb , kwa matumizi ya kawaida kabisa pia fuata vigezo hapo juu lakini itapendeza kama utachukua computer yenye ukubwa wa wastani ili kuifadhi kumbukumbu zako rahisi na kwa wingi Zaidi

Unaweza ukawa na home network nzuri inayo weza kukidhi mahitaji yako kabisa kwa kutumia simu yako ya smart phone, Hapa inakuwa haina haja ya kutumia modem kutengeneza network nyumbani hata oficine ,Kupitia simu yako ya smartphone unaweza kutengeneza wireless inayo weza kumudu kwa computer Zaidi ya tatu hadi nne kikubwa ni kujiunga vifurushi vya internet kama kawaida ya vifurushi vya mitandao yote alafu tengeneza wireless yako ufurahie internet na yenye kasi Zaidi



Jinsi ya kutengeneza wireless kwa kutumia smartphone yako fuata hatua zifuatazo 

Hatua ya kwanza
Ingia Katika sehemu ya setting kwenye simu bofya Mahali pameandikwa More..Utaona  maelezo haya juu kabisa pameandikwa Wireless&Networks chini yake utaona
Airplane Mode
Vpn Settings
Tethering & Portable hotspot
Mobile Networks

Hatua ya pili
Bofya mahali wameandika Tathering & Portable hotspot itakuonesha jinsi ya kuiwasha wireless yako lakini kabla ya yote unahitaji kuitengeneza kwa jina unalo taka kwa kubofya mahali pameandikwa Set-up Wi-Fi hotspot ,Andika jina upendalo pia kuna mahali pa kuweka passwork kama unahitaji kwa jili ya kuzuia watu wengi kutumia wireless yako basi andika passwork na iwe siri kwako tu ,Endapo utasambaza password yako utaona matumizi yako ya bundle ni makubwa kwa sababu utakuwa umeruhusu watu wengi watumie wireless yako

Hizo hatua mbili juu ni kwa wale watu wanao tumia simu za Android lakini kwa wanao tumia windows phone ni rahisi Zaidi kwani utaenda mahali pameandikwa setting halafu Internet sharing,Uta seti password na jina la wireless yako.
Kabla ya kufanya yote hayo hakikisha computer yako ina support wireless kama hapana basi angali kama kuna driver za wireless kama computer itakuwa hai support basi zoezi hili litakuwa gumu kwako.

Asante sana mpenzi msomaji wa Makala yangu hii ya leo mungu akubariki usikose kusoma habari nyingi Zaidi na Zaidi mada zinazo kuja mbele ni nzuri Zaidi tutafundisha jinsi ya kuinstall windows katika computer yako ,jinsi ya kuiandaa flash yako iweze kuboot window moja kwa moja badala ya kutumia CD” Mimi mwandishi wako henry Lameck unaweza wasiliana nami moja kwa moja katika email yangu hapa chini
pia +255765327325
      +255766518985
 
 



















 






1 comment:

  1. Technologia Ya Computer ~ Computer Services >>>>> Download Now

    >>>>> Download Full

    Technologia Ya Computer ~ Computer Services >>>>> Download LINK

    >>>>> Download Now

    Technologia Ya Computer ~ Computer Services >>>>> Download Full

    >>>>> Download LINK HC

    ReplyDelete

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

CHAT BOX

Post zilizo tumwa

Recent Posts Widget

Tangaza Biashara yako mtandaoni

TANGAZA BIASHARA NAMI HAPA KWA BEI NAFUU KABISA

Unaweza kutangaza biashara yako sasa na hlmservice pia uta pata kujua mambo mengi ambayo mbali na biashara yako unaweza ukatengeneza pesa kwa namna moja ama nyingine kama jinsi nilivo elezea katika Makala za nyuma hapo

Wafanya biashara wengi wanatumia mda mwingi namna gani ya kukuza biashara zao ,Ili uweze kufanikiwa kwa kiasi kikubwa unahitaji kuitangaza biashara yako ili kuwa na mtandao mkubwa na wateja wako ,ni vyema ukatangaza biashara yako katika mitandao ili bidhaa zako zijulikane kwa haraka na upesi .

Pia wewe mfanya biashara ukiitaji kuwa na blog yako wasiliana nami kwa mawasiliano hapo chini , bei ni nafuu kabisa

Pia ukiitaji kuitangaza biashara yako kupitia blog yangu bei ni ndogo kabisa huu ni wakati wako wewe mfanya biashara

+255758061575 & +255684860817

henrylameck@gmail.com

henrylameck90@yahoo.com

Tukuyu Tour & Safari

Vadacom Ni Zaidi

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Kilimo Kwanza

Hlm servise

Latest movie

Movies

Computer books

Computer books