umojannguvu.blogspot.com

Friday 21 August 2015

Msajili avionya vyama kampeni zenye vurugu




MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi ameviagiza vyama vya siasa kudhibiti vitendo vya wanachama wake vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani, ikiwamo tabia iliyojitokeza ya baadhi ya wanachama na mashabiki wa vyama hivyo kuwazomea na hata kuwarushia mawe wanachama na mashabiki wa vyama vingine, hasa pale wanapovaa sare za vyama vyao.

Amesema vyama vya siasa vina wajibu wa kijamii na kisheria wa kudhibiti vitendo hivyo. Katika taarifa yake kwa umma jana, Jaji Mutungi alisema amevitaka na kuviagiza vyama vyote vya siasa, kutoa maelekezo kwa wanachama wake wote na kuwataka wawe na utulivu katika kipindi chote cha Uchaguzi kwa kuheshimu sheria na kuzingatia dhana ya kufanya siasa za kistaarabu ikijumuisha kuwa na uvumilivu wa kisiasa.

“Siku za hivi karibuni kumejitokeza tabia ya baadhi ya wanachama na mashabiki wa baadhi ya vyama vya siasa kuwazomea na hata kuwarushia mawe wanachama na mashabiki wa vyama vingine na hasa pale wanapovaa sare za vyama vyao,” alisema Jaji Mutungi.

Jaji Mutungi alisema katika kipindi cha uchaguzi ni kipindi ambacho kuna ushindani mkubwa na matukio mengi ya kisiasa, hali ambayo inahitaji vyama vya siasa kuzingatia sana utii wa sheria za nchi na kufanya siasa za kistaarabu, ili kujiepusha na vitendo/matendo yanayoashiria uvunjifu wa amani.

Pia alisema anaamini kuwa migongano na migogoro baina ya vyama vya siasa au baina ya vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi. “Navitaka na kuviagiza vyama vyote vya siasa kutoa maelekezo kwa wanachama wake wote na kuwataka wawe na utulivu katika kipindi chote cha Uchaguzi kwa kuheshimu Sheria na kuzingatia dhana ya kufanya siasa za kistaarabu ikijumuisha kuwa na uvumilivu wa kisiasa,” alisema Msajili wa Vyama vya Siasa.

“Nawasihi wadau wengine wote ambao ni wapenzi wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa na ambao wangependa kuona nchi yetu ikimaliza kipindi hiki cha Uchaguzi kwa amani, basi wasisite kutoa taarifa kwa mamlaka husika punde wanapoona mfuasi, mwanachama au kiongozi wa chama anafanya vitendo vya ukiukwaji wa sheria kuhusiana na masuala ya kisiasa na uchaguzi.”

Kauli ya Jaji Mutungi imekuja huku Polisi wa Kanda ya Dar es Salaam wakitoa onyo kwa watu wanaojihusisha na vitendo vya kuzomea waliovalia sare za vyama na kusema hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alizungumzia vitendo hivyo vya kuzomea na kusema, kinachofanyika sasa, ni kufuatilia baadhi ya picha zilizosambaa kwenye mitandao zikionesha matukio hayo, kubaini wahusika wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.



Picha hizo zilionesha baadhi ya watu walio waliovalia sare za chama kimoja cha siasa, wakizomewa na umati wa vijana ingawa haikufahamika mara moja, eneo ambako vitendo hivyo vilifanyika. Kamanda Kova alisema mtu yeyote anayo haki ya kuvaa nguo ya rangi yoyote bila kubughudhiwa.
 
Kuhusu kampeni, Kova alihimiza wanasiasa kufanya kampeni za amani na kuasa viongozi wa vyama vya siasa kuendesha kampeni za kistaarabu pamoja na kuonya wafuasi wao wanapokwenda kinyume.

Kwa mujibu wa Kova, katika baadhi ya vyama, kunadaiwa kuundwa makundi ya ushabiki yanayolenga kuleta vurugu kwenye mikutano ya vyama pinzani. Viongozi wa dini na siasa Katika hatua nyingine, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imewakumbusha viongozi wa dini nchini kutoonesha hisia za kisiasa na kuepuka kushawishi waumini wao kuegemea upande wowote wa chama au mgombea katika kampeni zinazoanza kesho.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damiani Lubuva wakati wa mkutano kati ya Tume na viongozi wa dini katika kuwaelezea maandalizi ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.

Jaji Lubuva aliwataka viongozi hao wanapotoa mafundisho ya uchaguzi kutoonesha hisia kwa upande wowote wa chama cha siasa na zaidi kuepuka kuwashawishi waumini kuegemea upande wowote wa chama au mgombea.

Alisema viongozi wa dini wanao wajibu wa kutumia majukwaa yao kuelimisha na kufahamisha wapiga kura ili waweze kufanya maamuzi baada ya kupata taarifa sahihi na si kuruhusu wanasiasa kuyatumia majukwaa hayo ya dini kufanyia kampeni.

Alisema sheria za uchaguzi zinakataza viongozi wa dini kutumika katika masuala ya kisiasa kama vile kufanya kampeni za uchaguzi katika maeneo ya ibada. Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Kailima Ramadhani alisema jana kuwa, Tume haijatoa ratiba ya kampeni kutokana na baadhi ya vyama kutopeleka rasimu ratiba ya kampeni.

Alisema ni vyama vitatu ndiyo vilivyowasilisha ratiba, ikiwemo CCM inayozindua kampeni zake Jumapili jijini Dar es Salaam. Chadema haijatangaza siku ya kuzindua kampeni zao.

0 comments:

Post a Comment

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

CHAT BOX

Post zilizo tumwa

Recent Posts Widget

Tangaza Biashara yako mtandaoni

TANGAZA BIASHARA NAMI HAPA KWA BEI NAFUU KABISA

Unaweza kutangaza biashara yako sasa na hlmservice pia uta pata kujua mambo mengi ambayo mbali na biashara yako unaweza ukatengeneza pesa kwa namna moja ama nyingine kama jinsi nilivo elezea katika Makala za nyuma hapo

Wafanya biashara wengi wanatumia mda mwingi namna gani ya kukuza biashara zao ,Ili uweze kufanikiwa kwa kiasi kikubwa unahitaji kuitangaza biashara yako ili kuwa na mtandao mkubwa na wateja wako ,ni vyema ukatangaza biashara yako katika mitandao ili bidhaa zako zijulikane kwa haraka na upesi .

Pia wewe mfanya biashara ukiitaji kuwa na blog yako wasiliana nami kwa mawasiliano hapo chini , bei ni nafuu kabisa

Pia ukiitaji kuitangaza biashara yako kupitia blog yangu bei ni ndogo kabisa huu ni wakati wako wewe mfanya biashara

+255758061575 & +255684860817

henrylameck@gmail.com

henrylameck90@yahoo.com

Tukuyu Tour & Safari

Vadacom Ni Zaidi

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Kilimo Kwanza

Hlm servise

Latest movie

Movies

Computer books

Computer books