umojannguvu.blogspot.com

Thursday 20 August 2015

Marufuku kufanya siasa Uwanja wa Taifa




Serikali imepiga marufuku vyama vya siasa kufanya shughuli za kisiasa katika uwanja wa taifa na kusisitiza, utabaki kwa ajili ya michezo pekee.

Aidha, imekanusha taarifa za kwenye mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari kwamba, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kitafanya mkutano wake wa kufungua kampeni katika uwanja wa taifa.

Ufafanuzi huo ulitolewa jana na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Assah Mwambene wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam.
Alisema, hakuna chama chochote kitakachoruhusiwa kutumia uwanja huo kwa shughuli za siasa.

“Naomba niseme kwa sasa serikali haijaruhusu na hatutaruhusu chama chochote cha siasa kufanya shughuli za kisiasa katika uwanja wa Taifa, uwanja huu utabaki kwa ajili ya shughuli za michezo tu,” alisema Mwambene.

Mwambene alikiri kwamba, Chadema waliandika barua Agosti 12, mwaka huu kwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuomba kufanya mkutano wa ufunguzi wa kampeni zao, Agosti 22.

Alisema waliijibu barua kwa kuwaambia kwamba, uwanja huo upo kwa ajili ya shughuli za michezo na kwamba kwa mazingira ya sasa, hawaruhusu mihadhara ya vyama vya siasa kufanyika katika uwanja huo.

“Haturuhusu Uwanja wa Taifa kutumika kwa mihadhara ya kampeni za vyama vya siasa. Uamuzi huu unalenga kuweka uwanja katika mazingira rafiki ya michezo na kuepuka athari zozote zinazoweza kujitokeza kutokana na mihemuko ya kisiasa,” alisema Mwambene.

 



0 comments:

Post a Comment

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

CHAT BOX

Post zilizo tumwa

Recent Posts Widget

Tangaza Biashara yako mtandaoni

TANGAZA BIASHARA NAMI HAPA KWA BEI NAFUU KABISA

Unaweza kutangaza biashara yako sasa na hlmservice pia uta pata kujua mambo mengi ambayo mbali na biashara yako unaweza ukatengeneza pesa kwa namna moja ama nyingine kama jinsi nilivo elezea katika Makala za nyuma hapo

Wafanya biashara wengi wanatumia mda mwingi namna gani ya kukuza biashara zao ,Ili uweze kufanikiwa kwa kiasi kikubwa unahitaji kuitangaza biashara yako ili kuwa na mtandao mkubwa na wateja wako ,ni vyema ukatangaza biashara yako katika mitandao ili bidhaa zako zijulikane kwa haraka na upesi .

Pia wewe mfanya biashara ukiitaji kuwa na blog yako wasiliana nami kwa mawasiliano hapo chini , bei ni nafuu kabisa

Pia ukiitaji kuitangaza biashara yako kupitia blog yangu bei ni ndogo kabisa huu ni wakati wako wewe mfanya biashara

+255758061575 & +255684860817

henrylameck@gmail.com

henrylameck90@yahoo.com

Tukuyu Tour & Safari

Vadacom Ni Zaidi

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Kilimo Kwanza

Hlm servise

Latest movie

Movies

Computer books

Computer books