umojannguvu.blogspot.com

Sunday 23 August 2015

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amemsuta kiongozi wa upinzani wa Kenya, Raila Odinga, kwa kupinga mkataba wa uuzaji wa sukari uliotiwa sahihi majuzi.





Museveni alisema kuwa Odinga hafaaamu anachokisema.

''hata ndugu yangu odinga anazungumzia maswala ya sukari,bila kufahamu ukweli wa maswala hayo'' Museveni.

Kenya imekuwa ikizuia sukari yetu na mahindi ilihali Uganda imekuwa ikiagiza bidhaa za thamani kubwa pasi na kujali kuwa inawasaidia kujiendeleza.

''Wewe ni mkurugenzi wa kampuni ilihali kazi yako kubwa ni kuzuia sukari ya Uganda isiingie Kenya.

 

Hii ni akiligani jamani ?''aliuliza Museveni.

'Nafikiri nitampigia Raila simu nimwambie kuwa sukari ya Uganda itaingia Kenya sawa na vile mali ya Kenya inaingia Uganda bila vizingiti' aliongezea Museveni.

Rais Museveni aliyasema hayo alipokuwa akihutubia wageni waalikwa na wabunge wa bunge la Afrika Mashariki lililoanza vikao vyake jiji Kampala Uganda.

Museveni alisema mataifa wanachama wa muungano wa kanda hii ya Afrika Mashariki na kati sharti yafuate kanuni za muungano ikiwemo Kenya.

 

''Kenya inasafirisha mali ya thamani ya dola milioni 700 kuingia Uganda na kununua bidhaa zenye thamani ya dola milioni 150 kutoka Uganda, Ninamshukuru rais Kenyatta kwa kuondoa mashrti makali na vizuizi vilivyokuwa vinakataza bidhaa za Uganda Kuingia Kenya.alisema Museveni.
Uganda kwa sasa inasaga sukari tani 450,000 huku ikitumia takriban tani 320,000 na hivyo inasalia takriban tani 145,000 za sukari.

Hii ndiyo sukari ambayo sasa itaruhusiwa kuuzwa nchini Kenya.
Kwa Upande wake Kenya inazalisha takriban tani 600,000 ya sukari huku ikihitaji kati ya tani 800,000 na 850,000 kwa hivyo inanakisi ya takriban tani 250,000 za sukari kukidhi mahitaji ya raia wake.


Bwana Odinga amekuwa akidai kuwa sukari iliyokubalika kuingia Kenya kutoka Uganda sio sukari inayoundwa nchini humo bali ni sukari inayotokea Brazil na kupakiwa katika magunia ya sukari ya makampuni ya kusaga sukari ya uganda kwa minajili ya kukwepa kulipa kodi.

Wazo hilo limepuziliwa mbali na serikali ya Kenya ambayo imekuwa ikisisitiza kuwa sukari ya Uganda itaendelea kuingia Kenya chini ya mpango wa jumuia ya Afrika Mashariki COMESA.

0 comments:

Post a Comment

Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

CHAT BOX

Post zilizo tumwa

Recent Posts Widget

Tangaza Biashara yako mtandaoni

TANGAZA BIASHARA NAMI HAPA KWA BEI NAFUU KABISA

Unaweza kutangaza biashara yako sasa na hlmservice pia uta pata kujua mambo mengi ambayo mbali na biashara yako unaweza ukatengeneza pesa kwa namna moja ama nyingine kama jinsi nilivo elezea katika Makala za nyuma hapo

Wafanya biashara wengi wanatumia mda mwingi namna gani ya kukuza biashara zao ,Ili uweze kufanikiwa kwa kiasi kikubwa unahitaji kuitangaza biashara yako ili kuwa na mtandao mkubwa na wateja wako ,ni vyema ukatangaza biashara yako katika mitandao ili bidhaa zako zijulikane kwa haraka na upesi .

Pia wewe mfanya biashara ukiitaji kuwa na blog yako wasiliana nami kwa mawasiliano hapo chini , bei ni nafuu kabisa

Pia ukiitaji kuitangaza biashara yako kupitia blog yangu bei ni ndogo kabisa huu ni wakati wako wewe mfanya biashara

+255758061575 & +255684860817

henrylameck@gmail.com

henrylameck90@yahoo.com

Tukuyu Tour & Safari

Vadacom Ni Zaidi

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Tembelea g2g.fm upate movie Kali

Kilimo Kwanza

Hlm servise

Latest movie

Movies

Computer books

Computer books